February 4, 2021

 


UONGOZI wa klabu ya Yanga umesema unajivunia mafanikio makubwa waliyoyapata msimu huu kwa kutwaa taji la kombe la Mapinduzi, pamoja na kuongoza msimamo wa Ligi Kuu Bara mpaka sasa.

Yanga mpaka sasa ndiyo timu pekee ambayo haijapoteza mchezo kwenye ligi, ambapo wamejikusanyia pointi 44 baada ya kucheza michezo 18,  wakishinda mechi 13 na kutoa sare michezo mitano pekee.

Akizungumzia mipango na mafanikio yao msimu huu Mkurugenzi wa uwekezaji wa GSM na mjumbe wa kamati ya usajili ya Yanga, Injinia, Hersi Said amesema: “Tumefanya uwekezaji mkubwa ndani ya kikosi chetu msimu huu, na sisi sote tunakubaliana kwamba tayari matunda yameanza kuonekana kupitia ubingwa wa mapinduzi na mwenendo mzuri kwenye ligi.

“Tunashukuru Mungu katika hilo na wakati huu tumebaki na lengo moja tu la kuhakikisha tunaibuka mabingwa msimu huu.


11 COMMENTS:

  1. Words my brother!! Kuna timu hapa bila mchezaji flani kucheza hamna kitu milele

    ReplyDelete
  2. Ujinga wa kutambia Mapinduzi Cup. Azam kachukua mara 5 husikii wakisema ni mafanikio!!!
    Mapinduzi Cup imekuwa mafanikio???

    ReplyDelete
  3. Kuongoza ligi mmeongoza kwa miaka 3 lakini bingwa anajulikana.

    ReplyDelete
  4. Mapinduzi na Simba super cup Nani zaidi?

    ReplyDelete
    Replies
    1. Mapinduzi "big up" sio la maigizo

      Delete
  5. Sasa mbona yule Bonjour katamba nalo?,shida hapa ni uelewa na age .Hata Hiyo Mapinduzi ukiangalia Wananchi tulibaka walishandaa Bingwa wao ndiyo maana eti Opiyo Mchezaji Bora?,tukaharibu mpango hata Ile Hundi mfano ya Mchezaji Bora ukiangalia Tarakimu Ile ya mwanzo ni Kama iliandikwa palepale Uwanjani najua wengi hamkuiona.Inawezekana waliandaa laki tano wakijua Paka atakuwa Bingwa baada ya kukosa wakabadili figure ili wawaridhishe makauzu (Zingatia haikuwa na maneno Ila Tarakimu tu)

    ReplyDelete
  6. Daah kweli maisha yanakwenda kasi Sana leo hii yanga kuongoza ligi kwao ni mafanikio makubwa.... Kweli Mnyama amewapoteza vibaya

    ReplyDelete
  7. Kombe la mapinduzi kwa njia ya bahatinasibu kwa panelti ndio mafanikio makubwa kwa matopolo ambayo wanayoyataja kila kukicha. Wanasema hiyo ndio fahari yao na jee pindi wakibahatika kupata ubingwa tungojee tuone tuombe salama

    ReplyDelete
  8. Do 90 no single shot on target Nani alikuwa anangoja Penalt?Hilo huwa hamjibu.

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic