MIAMBA ya soka kutokea nchini Afrika Kusini, Kaizer Chiefs
wameonyesha nia ya kumsajili mshambuliaji wa klabu ya Simba raia wa Nigeria,
Junior Lokosa, ambapo inaelezwa Simba wanahitaji dau la dola 200,000 sawa na
zaidi ya Shilingi Milioni 464.
Lokosa alijiunga na Simba kwenye dirisha la usajili la mwezi Januari, lakini tangu atue ndani ya kikosi cha timu hiyo ameonekana kupata wakati mgumu kuingia kwenye kikosi cha kwanza cha Simba, mbele ya Chris Mugalu ambaye ndiye chaguo la kwanza la kocha, Didier Gomes.
Inaelezwa kuwa kikosi cha Strømsgodset Toppfotball ya nchini
Norway, kilichoonyesha nia ya kumuhitaji nyota huyo kimejiondoa kwenye mpango
huo.
Akizungumzia ofa hiyo ya Kaizer Chief, Katibu Mkuu wa Simba,
Dk Arnold Kashembe amesema: “Sijapokea taarifa zozote kuhusiana na ofa ya klabu ya Kaizer
Chief kumtaka mshambuliaji wetu, Junior Lokosa.
“Hivyo siwezi kusema lolote kwa sasa lakini iwapo kutakuwa na
taarifa yoyote rasmi kuhusiana na hilo basi tutawaeleza,”
Lokosa mchezaji simba wamstahilie
ReplyDeleteAndika vizuri tukuelewe
DeleteJuzi nilisoma mahali kwamba mmevunja nae mkataba
ReplyDelete