KIKOSI cha klabu ya Yanga leo kimefanya mazoezi yao ya mwisho
kuelekea mchezo wao wa kesho dhidi ya Coastal Union huku wakitamba kufanya
vizuri katika mchezo huo.
Mchezo huo unatarajiwa kupigwa katika dimba la Mkwakwani,
jijini Tanga majira ya saa 10 kamili jioni.
Yanga wametamba kuwa, ushindi wa bao 1-0 walioupata kwenye
mchezo uliopita dhidi ya Kengold, katika michuano ya kombe la Shirikisho
umezidi kuamsha ari ya kushinda mchezo wa kesho.
Akizungumzia maandalizi yao kuelekea mchezo huo, Ofisa Mhamasishaji
wa Yanga, Antonio Nugaz amewaomba Wanayanga kujitokeza kwa wingi, ili kuwapa
sapoti wachezaji wa kikosi hicho.
“Kikosi chetu kimekamilisha mazoezi ya mwisho leo kuelekea
mchezo wa kesho dhidi ya Coastal Union.
“Ni wazi ushindi tulioupata katika mchezo uliopita dhidi ya Kengold
kwenye michuano ya kombe la FA, umezidi kutupa ari ya kufanya vizuri kwenye
mchezo huu,”
Coastal tandika hap malalamiko fc ili wanitoe vizuri kwenye ligi
ReplyDeleteIli wajitoe
ReplyDeleteTawi lenu mikia aka paka mweusi
ReplyDeleteTFF iwamilike fujo za makomandoo wao
ReplyDeleteUtopolo leo presha kama yote... Yanagonga yanarudi. Kichapo kinawahusu leo wakijitahidi saaana wanapata sare
ReplyDelete