April 16, 2021


ACHANA na ushindi wa mabao 5-0 walioupata

Simba, juzi katika mchezo dhidi ya Mtibwa

Sugar, jambo la ziada ni kwamba ushindi huo

umewafanya nyota wawili wa kikosi cha Simba,

Meddie Kagere na Clatous Chama kuandika

rekodi ya aina yake kwenye Ligi Kuu Bara

(VPL).

 

Katika mchezo huo wa juzi nyota hao wawili

walihusika katika mabao manne ambapo,

Kagere alifunga mabao mawili huku Chama

yeye akifunga bao moja na kuasisti bao moja.

 

Kutokana na mabao hayo Chama sasa

ameivunja rasmi rekodi yake ya msimu uliopita

ambapo kwenye Ligi Kuu Bara pekee msimu huu, Chama amehusika kwenye mabao 17

akifunga mabao saba na kuasisti mara 10.

 

Msimu uliopita Chama alihusika kwenye mabao

15 ya michuano yote, ambapo kwenye Ligi Kuu

Bara alifunga mabao mawili na kuasisti mara

10.

 

Kwa upande wa Kagere mabao yake mawili

yamemfanya afikishe mabao 56 tangu atue

ndani ya Ligi Kuu Bara, ambapo huu ni msimu

wa tatu kwake tena akifanikiwa kufunga mabao

zaidi ya 10 kwa msimu.

 

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic