HAKUNA kisingizio Septemba 25
kwenye mchezo wa Ngao ya Jamii ambao utakuwa ni ufunguo wa msimu mpya wa Ligi
Kuu Bara 2021-22, Simba na Yanga wakishuka dimbani.
Utamu wa mchezo unazidi
kuongezeka kutokana na vikosi vyote viwili kuonekekana kuimarika zaidi kutokana
na usajili ambao umefanywa hadi sasa kwa kila upande.
Yanga waliteswa sana na eneo la
ushambuliaji msimu uliopita, na ndiyo maana kwenye dirisha hili la usajili
wamecheza zaidi kwenye eneo hilo kwa kusajili nyota ambao wanaamini wataleta
mabadiliko.
Kwa usajili wa timu zote ambao
umefanyika hadi sasa, Yanga wanaonekana kuimarika zaidi kwenye eneo la mbele
wakiwa na maingizo mapya, Fiston Mayele, Heritier Makambo, Jesus Moloko na
Dickson Ambundo.
Ambao wanakwenda kuungana na
nyota kama Deus Kaseke, Ditram Nchimbi na Yacouba Sogne.
Wakati Yanga wakitamba na
washambuliaji zaidi, Simba wao hawakuwa na shida sana kwenye eneo hilo baada ya
kuwepo nyota kama John Bocco, Chris Mugalu na Meddie Kagere.
Wao wakaamua kucheza na viungo
zaidi, wakimleta Peter Banda, Duncan Nyoni, Ousmene Sakho, Abdulswamad
Kassim,na Sadio Kanoute ambao wanakwenda kuungana na Tadeo Lwanga, Jonas Mkude,
Said Ndemla, Hassan Dilunga na Raly Bwalya.
Hata hivyo ukiachana na timu zote
kutamba na usajili wao huo msimu huu,timu hizo hadi sasa kutokana na sajili
walizozifanya wamefanikiwa kutengeza vikosi viwili hatari yaani kikosi cha
kwanza na cha pili, vyote kuonekana kuwa hatari.
Kwa upande wa Yanga wao kikosi
chao cha kwanza chini ya kocha Nadreddine Nabi kinatarajiwa kuwa hivi 1.Diarra
Djigui 2.Djuma Shabani 3.David Bryson, 4.Bangala Litombo 5.Bakari Mwamnyeto
6.Mukoko Tonombe 7.Feisal Salum, 8.Khalid Aucho, 9.Heriter Makambo, 10.Fiston
Mayele, 11.Yacouba Songne
Kikosi cha pili cha Yanga
kinatarajiwa kuwa na nyota hawa kipa 1.Erick Johora 2.Kibwana Shomari, 3.Yasin
Mustapha 4. Abdallah Shaibu Ninja, 5.Dickson Job, 6.Zawadi Mauya, 7.Ducapel
Moloko, 8.Deus Kaseke, 9.Yusuph Athumani, 10.Saido Ntibazonkiza, 11.Dickson
Ambundo.
Watakaosubiri ni Ramadhani
Kabwili, Adeyum Salehe, Balama Mapinduzi, Paul Godfrey Boxer, Farid Mussa na Ditram
Nchimbi.
Kwa upande wa kikosi cha pili cha Simba chenyewe kinatarajiwa kuwa hivi 1.Beno Kakolanya, 2.Isra Mwenda3. Gadiel Michael, 4.Erasto Nyoni, 5.Henock Baka, 6.Jonas Mkude, 7.Bernard Morrison, 8.Sadio Kanoute, 9.Meddie Kagere 10.Yusuph Mhilu 11.Duncun Nyoni.
Wanaobaki katika kikosi cha Simba
watakuwa ni Jeremia Kisubi,Perfect Chikwende,Hassan Dilunga,Said
Ndemla,Abdulswamad Kassim,Mzamiru Yassin,Ibrahim Ame,Kibu Denis.
Jimmyson Mwanuke aliyesajiliwa juzi juzi tu atatolewa mkopo?????
ReplyDeleteMwinuke hatolewi kwa mkopo umri sio sababu ya mchezaji kutolewa kwa mkopo. Mwinuke ni kijana mwenye kipaji maalum licha ta umri wake kuwa Mdogo akikaza atatoboa mapema tu wanaomsimia wanatakiwa kumtafutia daftari la Mbwa samata ndani ya Simba.
ReplyDelete