MSEMAJI wa Yanga, Haji Manara
amefunguka kuwa wingi wa makombe ambayo alikuwa akiyazungumza akiwa Simba
unajumuisha michuano ambayo ilikuwa ni ya mabonanza.
Agosti 24, mwaka huu kupitia
mkutano na waandishi wa habari, Yanga ilimtambulisha rasmi Manara kuwa msemaji
wao mpya, huku zikiwa zimepita siku chache tangu aachwe na Simba.
Tangu kuondoka kwake ndani ya
Simba, Manara mara kwa mara amekuwa akizungumza kauli zenye tafsiri ya utata
kuwahusu baadhi ya viongozi wa Simba, na klabu hiyo.
Akizungumza katika kituo kimoja
cha redio kuhusu utumishi wake ndani ya Simba, Manara amesema: “Moja ya kazi
kubwa ambayo niliifanya labda ni kuonesha ukubwa feki, hiyo dhambi niliitendea
vibaya sana Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na nipo tayari kuhukumiwa hata
gerezani kwa kufanya ulaghai wa ukubwa ambao haupo.
“Nazungumzia uhalisia, mimi siku zote sijawahi
kuwa Simba, mimi nilikuwa Yanga.”
Kuhusu wingi wa makombe ya Simba
“Unajua sisi watu wengi ambao tupo kwenye mpira huwa hatuzungumzi uhalisia, lakini narudia tena unaposimamia takwimu basi Yanga ndiyo klabu yenye mataji mengi ya Ligi Kuu hapa nchini, lakini pia ndiyo klabu yenye makombe mengi zaidi hapa nchini.
“Kuna watu wengine wataanza kuuliza mbona ulivyokuwa Simba ulitoa takwimu tofauti, watu wanapaswa kutofautisha porojo na uhalisia, unajuaje kama labda nilizungumza nikiwa nimelewa, na huo ndio uhalisia kama utahusisha na takwimu za makombe ya mabonanza.”
Ubingwa wa Sinba viwanjani na hiyo iwe shabaha. Simba inaataka vitendo sio ulimi wa kujibizana kulikopitwa na wakati
ReplyDeleteKeshakywa chizi huyu, haamini kama katemwa simba
ReplyDeleteYanga bado wanafurahia kombe la amapinduzi😆
ReplyDeleteNilifikili Ni Kombe la karafuu ndilo linaitwa la mapinduzi Zanzibar
DeleteMakolo acha awape za uso na bado picha lenyewe..hahaha
ReplyDeleteMakolo ni jina la mtu pale Upareni hivyo kawaulize wapare watakupa maana ya jina la Makolo
DeleteUsajili wa wacheza ndombolo na manara awe.dj
ReplyDeleteManara kuwa na akiba ya maneno,usitukane wakunga...........
ReplyDelete