September 10, 2021


 BAADA ya ratiba ya Ngao ya Jamii kuwa wazi na ikitarajiwa kuchezwa Septemba 25 kati ya Simba v Yanga, leo Bodi ya Ligi Tanzania, (TPLB) imeweka hadharani ratiba ya ligi.

Ratiba inaonyesha kwamba Ligi Kuu Bara inatarajiwa kuanza rasmi Septemba 27 ambapo ni Mtibwa Sugar v Mbeya Kwanza, Uwanja wa Jamhuri, Moro.

Namungo v Geita utapigwa Uwanja wa Ilulu.

Coastal Union v Azam FC, Uwanja wa Mkwakwani, Tanga.

Hizi hapa zitapigwa Septemba 28:-

Dodoma Jiji v Ruvu Shooting, Uwanja wa Jamhuri, Dodoma.

Mbeya City v Mbeya City ngoma itapigwa Uwanja wa Sokoine, Mbeya.

Biashara United v Simba SC, Uwanja wa Karume, Mara.

Polisi Tanzania v KMC ngoma itapigwa Uwanja wa Ushirika, Moshi.

Kagera Sugar v Yanga ngoma itapigwa Uwanja wa Kaitaba.

Yanga na Simba hizi mechi zao za ufunguzi zote watakuwa ugenini huku mchezo wao wa Kariakoo Dabi kwenye ligi ukitarajiwa kuchezwa tarehe 11/12/2021.

9 COMMENTS:

  1. Mbeya City vs Prisons

    ReplyDelete
    Replies
    1. Nilikuwa najiuliza labda itakuwa Mbeya City A vs Mbeya City B

      Delete
  2. Hivi Haji Manara anashida gani?????

    ReplyDelete
  3. Haji Manara ameumizwa SANA Na SIMBA???

    ReplyDelete
    Replies
    1. Anaumia hadi amezeeka ghafla, huyu apewe uangalizi maana afya yake inatetereka kwa kuiwazia Simba

      Delete
  4. Ikitokea YANGA wanamwondoa Manara je hatakufa kwa presha????

    ReplyDelete
  5. Hapo ni manara vs manara maana hakuna anaye mjibu bas anajijibu mwenyew

    ReplyDelete
  6. Manara ni msakatonge na sivingine

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic