Mtibwa Sugar imefunga Simba bao 1-0
katika mechi ya kirafiki iliyopigwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es
Salaam, leo.
Pamoja na kipigo hicho, Kocha wa Simba,
Dravko Logarusic amesema wako kwenye mchakato wa kusaka kikosi, hivyo hawana
sababu ya hofu.
“Hakuna sababu ya kuwa na hofu, najua
kufungwa si kitu kizuri lakini ni kitu kizuri kwetu kwa kuwa tunajiandaa na
ligi.
“Hivyo tunajaribu kufanya kila
linalowezekana ili kuwa na kikosi bora kabisa, kufungwa kunatuumiza lakini
tukutumie kama njia sahihi ya kujifunza,” alisema Logarusic.
Katika mechi hiyo kocha huyo raia wa
Croatia, alifanya mabadiliko ya wachezaji wote walioanza katika kikosi cha
kwanza isipokuwa beki Kaze.
Mechi ilikuwa na ushindani wa juu na
Mtibwa Sugar ndiyo walioonyesha kiwango kizuri zaidi hasa kipindi cha pili.
Huu ni mchezo wa pili mfululizo
Logarusic kufungwa, mara ya mwisho Simba ililala bao 1-0 katika mechi ya
fainali ya Kombe la Mapinduzi dhidi ya KCC ya Uganda.
0 COMMENTS:
Post a Comment