Msemaji wa Mtibwa Sugar,
Thobias Kifaru amejigamba na kusema Simba anaifananisha na timu ya daraja la
kwanza.
Simba inakutana na Mtibwa
Sugar katika mechi yake ya sita ya Ligi Kuu Bara wikiendi hii kwenye Uwanja wa
Jamhuri mjini Morogoro.
Kifaru amesema wakiwa Mbeya
kabla ya kucheza na Mbeya City waliishuhudia Simba ikitoka sare ya mabao 1-1 na
Prisons.
“Simba ni timu isiyo na
mfumo mzuri, iliyojaza wachezaji wengi wageni wasio na msaada wowote.
“Sisi tunawachukulia kama
timu ya daraja la kwanza na tutawamaliza Morogoro pale Jamhuri, watu waje
waone,” alisema Kifaru.
Tayari Simba ina sare tano
wakati Mtibwa Sugar ndiyo timu inayoongoza kwa ushindi na inaonekana ni tishio
zaidi kuliko timu nyingine ya Ligi Kuu Bara kwa sasa.
0 COMMENTS:
Post a Comment