Mshambuliaji Mohammed Rashid anatarajia kuanza kuichezea Simba katika michuano ya SportPesa Super Cup inayoanza keshokutwa mjini Nakuru, Kenya.
Mohammed amejiunga na Simba akitokea Prisons na taarifa zinaeleza kwamba amemalizana na Simba jana usiku.
“Kweli wamemalizana na yeye sasa ni safari ya kwenda Kenya kwa ajili ya michuano ya SportsPesa,” kilieleza chanzo.
Hivi karibuni mshambuliaji huyo alikataa kuongeza mkataba na Prisons ingawa hakuwa amesema anataka kufanya nini.
Taarifa zinaeleza alikataa kuongeza mkataba mpya baada ya kukubaliana jambo na Simba, hivyo alikuwa akisubiri kumalizika kwa msimu.
Maamuzi mazuri yaliyofuata taratibu za mpira. Lakini nilisikia wachezaji wageni hawataruhusiwa kucheza kwenye mashindano hayo, kama ni kweli basi kuna kasoro katika kufikiri. Tatizo ninini kuwakataza wachezaji wageni? Ligi zao zimekwisha wamejiunga na timu mpya, kosa lipo wapi? Viongozi nipeni ufafanuzi.
ReplyDeletehakuna jambo kama hilo,wanacheza ndugu
Deletehakuna jambo kama hilo,wanacheza ndugu
DeleteAsante kwa kunipa amani
DeleteAnaejuwa ningependa atujuilishe sababu ya kutoshiriki idadi ya nyota wa Simba safari ya Kenya.
ReplyDelete