Searching...
Select a Page
  • MWANZO
  • KITAIFA
  • KIMATAIFA
  • MAKALA
  • BURUDANI
  • USAJILI
  • SALEHJEMBE TV
  • HABARI ZINGINE
    • TENNIS
    • GOLF
    • WWE
    • FOMULA ONE


Home » Kimataifa » SEVILLA KUTUA KESHO DAR, YALETWA NA SportPesa KUIVAA SIMBA
May 20, 2019

SEVILLA KUTUA KESHO DAR, YALETWA NA SportPesa KUIVAA SIMBA



TIMU ya Sevilla inatarajiwa kuwasili nchini Tanzania kesho Jumanne kwa ajili ya mchezo wa kirafiki ulioandaliwa na Kampuni ya SportPesa kwa ushirikiano wa La Liga.
Sevilla inatarajiwa kucheza mchezo huo wa kirafiki na Mabingwa wa Ligi Kuu Bara utakaopigwa Alhamisi ya wiki hii kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam saa moja kamili usiku.
Akizungumza na Waandishi wa Habari, Mkurugenzi wa Utawala na Udhibiti SportPesa Tanzania, Tarimba Abbas amesema “SportPesa inakwenda kuweka historia kwa mara nyingine tena nchini kwenye sekta ya soka kwa kuileta timu ya kimataifa ya Sevilla.
“Kupitia ujio wa timu ya Sevilla watafanya shughuli mbalimbali zenye lengo la kuinua sekta ya michezo nchini kwa vijana na soka kwa ujumla.
“Watatoa mafunzo ambayo yatahudhuriwa na timu ya vijana ya Bom Bom FC kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar bila kusahau semina elekezi itakayotolewa na maofisa wa klabu ya Sevilla kwa viongozi wa klabu, TFF na washirika wake ili wapate kuimarika kitaaluma na kupata uelewa jinsi ya kuongeza mapato,”amesema Tarimba.
Naye Mkurugenzi wa Mashindano wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Salum Madadi amemtaja mwamuzi wa kati wa kimataifa wa Tanzania, Herry Sassi ndiye aliyeteuliwa kuchezesha mchezo huo atakayesaidiana na Mohamed Mkono (Tanga), Soud Lila (Dar) huku mwamuzi wa akiba akiwa ni Jonesia Rukyaa (Kagera).
“Waamuzi wanaochezesha mchezo huu wote ni waamuzi wenye beji ya Fifa, mchezo huu mbali ya kujitangaza kama nchi lakini pia ni sehemu ya kutangaza vitu vyetu mbalimbali wakkiwemo wachezaji na waamuzi wetu,”amesema Madadi.
Kwa upande wa Simba, Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano wa timu hiyo, Haji Manara amesema kuwa “Bado tunaendelea kuwashukuru SportPersa kwa kufanikisha ujio wa Sevilla nchini, ni fursa ambayo kila timu ya soka Afrika ingetamani kuipata.
“Maandalizi ya mchezo huo na Sevilla yanaendelea vizuri, timu imeelekea Singida kwa ajili ya mchezo wa Ligi Kuu Bara tutakaocheza kesho huko Namfua na mara baada ya mchezo huo timu itarejea kwa ajili ya kujiandaa na pambano hilo,”amesema Manara.


ReplyForward
IMEWEKWA NA Dizo One @ 3:52 PM
Email ThisBlogThis!Share to XShare to Facebook
Labels: Kimataifa
Next
Newer Post
Previous
Older Post

0 COMMENTS:

Post a Comment

Subscribe to: Post Comments (Atom)

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV
B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic




JIUNGE NA SALEH JEMBE SPORTS INSTAGRAM, GONGA HAPA, UPDATES KAMA ZOTE

BONYEZA HAPA KUJIUNGA NASI INSTAGRAM! KWA UPDATES ZOTE ZA MICHEZO

JIUNGE NA MIMI HAPA

FACEBOOK

SPORTS GEAR & FOOTWEAR

SPORTS GEAR & FOOTWEAR

WADAU WA BLOG HII

ZILIZOSOMWA SANA

  • FT:LIGI KUU BARA: SIMBA 2-2 AZAM FC
      FT: Simba 2-2 Azam FC NGOMA imekamilika Uwanja wa Mkapa leo Februari 7 kwa Simba kugawana pointi mojamoja na wapinzani wao Azam FC. Dakika...
  • MUONEKANO WA UKURASA WA MBELE GAZETI LA CHAMPIONI IJUMAA
      MUONEKANO wa ukurasa wa mbele gazeti la Championi Ijumaa 
  • HAO SINGIDA BLACK STARS HAWANA UTANI, WAIPIGA MKWARA SIMBA
      UONGOZI wa Klabu ya Singida Black Stars umebainisha kuwa utapambana kuwaondoa wapinzani wao Simba katika hatua ya nusu fainali ili kutinga...
  • MAKAMBO ATOA RASMI TAMKO JUU YA YANGA NA HOROYA AC
    MSHAMBULIAJI wa Yanga Mkongomani, Heritier Makambo amewashukuru mashabiki wa timu hiyo kwa sapoti waliyompa katika kipindi cha mwaka mm...
  • VIDEO: UWANJA WA MKAPA KUFANYIWA MABORESHO MAKUBWA
    UWANJA wa Mkapa kufanyiwa maboresho makubwa, Msemaji wa Serikali Gerson Msigwa amebainisha mpango kazi  
  • ISHU YA SIMBA KUPELEKWA MAHAKAMANI IPO HIVI, MAWAKILI KAMA WOTE WAANDALIWA
      HAJI Manara aliyewahi kuwa Ofisa Habari wa Simba na sasa ni Ofisa Habari wa Yanga ameweka wazi kuwa ameandaa mawakiki 10 wa kusimamia kesi...
  • FOUNTAIN GATE WAITISHA YANGA HUKO
      WAPINZANI wa Yanga ndani ya Ligi Kuu Bara ambayo ni namba nne kwa ubora kuelekea kwenye mchezo wao unaotarajiwa kuchezwa Aprili 21 2025 Uw...
  • UBINGWA LIGI KUU ENGLAND SI MCHEZO
    VITA kubwa kwa sasa inayoendelea ndani ya Ligi Kuu England ni kujua nani atakuwa bingwa kwa msimu wa 2021/22 kutokana na kila timu kuonekana...
  • MASHABIKI RUKSA AZAM FC v PYRAMIDS FC KESHO
     KUELEKEA mchezo wa kesho wa Kombe la Shirikisho unaotarajiwa kuchezwa Uwanja wa AzM Complex kati ya Azam FC v Pyramids ya Misri mashabiki r...
  • WAMEANZA NA MAJANGA MSIMU MPYA WA 2021/22, SIMBA WANAWEZA KUKOSA UBINGWA
       IKIWA Simba watakuwa kwenye mwendo huu ndani ya msimu wa 2021/22 kengele ya hatari inawaka kwenye kichwa cha Kocha Mkuu, Didier Gomes kwa...
index.jpg
 
COPYRIGHT © SALEH JEMBE HAKI ZOTE ZIMEHIFADHIWA
BLOG DESIGNED BY SALEH JEMBE =>TANZANIA SPORTS
•