September 28, 2019



JOHN Bocco, nahodha wa Simba, msimu uliopita uwanja wa Karume aliwanyanyua mashabiki wa Simba kwa kufunga mabao 2 yaliyoipa pointi tatu Simba, hatakuwepo kesho jambo linalompasua kichwa, Kocha Mkuu, Patrick Aussems.

Simba itashuka uwanjani kesho kumenyana na Biashara United mchezo wake wa nne wa ligi bila Bocco ambaye anasumbuliwa na majeruhi ya goti aliyoyapata wakati Simba ikicheza na Azam FC mchezo wa ngao ya Jamii.

Aussems amesema kuwa miongoni mwa wachezaji muhimu ndani ya kikosi chake ni Bocco ila atalazimika kuendelea na mapambano bila uwepo wake.

“Unapozungumzia Simba kila mchezaji ana umuhimu wake hata Bocco pia ni muhimu hivyo kukosekana kwake ni pigo kwa timu kiujumla, tuna michezo mingi muhimu na malengo yetu ni kupata ushindi inanibidi niwape nafasi wengine,” amesema.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic