JKT Tanzania iliyo chini ya Kocha Mkuu, Mohamed Abdalah ‘Bares’
imegoma kufanya usajili msimu huu wa usajili wa dirisha dogo lililofunguliwa
Desemba 16.
Kwa sasa JKT ipo nafasi ya saba ina pointi 19 kwenye msimamo baada ya kucheza
mechi 13 ilishinda mechi tano na kupoteza mechi nne na kutoa sare nne.
Akizungumza na Saleh Jembe, Bares amesema kuwa kwa sasa wanatambua
dirisha limefunguliwa ila hawana presha ya kufanya usajili zaidi ya kuwatumia
wachezaji wake wa kikosi cha vijana.
“Nina kikosi cha vijana ambao wana uwezo mkubwa ndani ya timu
hvyo nitakachokifanya ni kuwapa nafasi wale ambao nitakuwa ninawahitaji kuhusu
usajili kwa sasa sifikirii kuwa na ingizo jipya.
“Ushindani ni mkubwa na kila mmoja anatambua kwamba ligi ya
msimu huu ni tofauti na msimu uliopita kikubwa ni kutambua kwamba wachezaji
wanamajukumu yao ndani ya uwanja na benchi la ufundi nalo linatimiza majukumu
yake kwa wakati,” amesema Bares.
0 COMMENTS:
Post a Comment