UONGOZI wa KMC umesema kuwa kwa sasa akili zao ni kwenye mchezo
wao wa ligi dhidi ya Simba utakaochezwa leo Desemba 28 uwanja wa Uhuru.
KMC ipo nafasi ya 17 imekuwa na msimu wa kusuasua kutokana na kushindwa kufurukuta kwenye
mechi 12 walizocheza ina pointi 9 ikiwa ilishinda mechi mbili pekee sare
tatu na kichapo saba.
Ofisa Habari wa KMC, Anwar Binde
amesema kuwa wanatambua kwamba hawajawa na msimu mzuri ila watapambana kurejea
kwenye ubora wao.
“Kila kitu ni hatua kwani hakuna mchezaji anayependa kupata
matokeo mabovu ila kutokana na ushindani na kipindi cha mpito tunakutana na
haya ila hatutapenda kuziacha pointi tatu mbele ya Simba ni muhimu kwetu na
tunapambana, mashabiki watupe sapoti,” amesema.
pole yenu coz simba nasi tunahitaji point zenu ety
ReplyDeleteHapana panic kwasababu mtazipata na Kocha Mkwasa keshasema kuwa Simba ni timu ya kawaida tu kwaahivo timu hizo mbili kila moja kwaurahisi mutapata point tatu tatu
ReplyDelete