June 26, 2020



YUSUPH Mhilu, mshambuliaji namba moja wa Klabu ya Kagera Sugar akiwa na mabao 12, chini ya Kocha Mkuu, Mecky Maxime amesema kuwa kilichowamaliza  wapinzani wao Azam FC ni kushindwa kutumia nafasi ambazo walizipata.

Kwenye mchezo huo uliochezwa Juni 24, Uwanja wa Kaitaba, Azam FC inayonolewa na Kocha Mkuu, Aristica Cioaba ilikubali kufungwa bao 1-0 baada ya kipa wa Azam FC, Benedict Haule kutema mpira uliokutana na guu la Mhilu.

Akizungumza na Saleh Jembe, Mhilu amesema kuwa ulikuwa mchezo mgumu na kila timu ilikuwa inahitaji ushindi hivyo kosa la Azam FC lilikuwa kushindwa kutumia nafasi walizotengeneza.

“Mchezo ulikuwa kwenye usawa, wao walikuwa wanatushambulia nasi tulikuwa tunawashambulia, kilichotufanya tukaweza kuwapunguzia kasi ni kosa lao moja walilofanya sisi tukatumia na kupata pointi tatu hakuna kingine,” amesema Mhilu.

Kagera Sugar, ipo nafasi ya nane ikiwa na pointi 44 huku Azam FC ikiwa nafasi ya pili na pointi zake 58 zote zimecheza mechi 31.

1 COMMENTS:

  1. Mhilu umeongea vizuri kwa kuwaheshimu wapinzani wenu hiyo ni safi sana kuheshimiana.

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic