August 12, 2020

 


MSHAMBULIAJI mpya wa Yanga, Wazir Junior, amesema anajisikia faraja kupata nafasi ya kucheza Yanga kwani aliweka ahadi kwa mama yake mzazi kabla hajafariki kuwa ipo siku atakuja kuwa mchezaji wa timu hiyo.

 

Wazir amesema mama yake alikuwa na mapenzi makubwa na Yanga enzi za uhai wake, hivyo kutokana na ushabiki huo wa mzazi wake kwa Yanga, akaamua kumpa ahadi kuwa ataongeza juhudi ili siku moja aweze kutua Jangwani.

 

Wazir amesajiliwa na Yanga kwa mkataba wa miaka miwili akitokea Mbao FC, kwa ajili ya msimu ujao wa Ligi Kuu Tanzania Bara, utakaoanza Septemba 6, mwaka huu. Wazir alimaliza msimu akiwa kinara wa mabao ndani ya Mbao akifunga mabao 13. Mama yake mzazi alifariki dunia miaka mitatu iliyopita.

 

Waziri amesema: “Nilimuahidi mama yangu kabla hajafariki ipo siku nitaichezea Yanga. Namshukuru Mwenyezi Mungu nilichomuahidi mama yangu kimetimia, japo yeye hayupo tena kwa sasa ila napata faraja kuona nimetimiza ahadi yake.


“Ndugu zangu pia ni wananchi. Kaka ni Mwanajangwani na mdogo wetu ana mapenzi makubwa na Yanga, hivyo kwao ni furaha baada ya kuona ndugu yao nipo kwenye timu wanayoipenda.”


1 COMMENTS:

  1. Waziri nambie Mzee Ally Shentembo alikua shabiki wa Manyani FC ama Mikia FC? Ongea ukweli mwanañgu

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic